Tuesday, July 30, 2024

TUOMBEE TAIFA LETU TANZANIA

Shalom karibu tena Tushiriki pamoja Neno la Bwana kutoka kwa bishop victory kiluguma .         1TIMOTHEO 2 :1-7.   Basi kabla ya mambo yote,nataka dua na sala,na maombezi,na shukurani,zifanyike kwaajili ya watu wote; 2 kwaajili ya wafalme na wote wenye mamlaka,tuishi maisha ya  amani,katika utsuwa wote na ustahivu.3 hili ni zuri,nalo lakubalika mbele za Mungu Mwokozi wetu; 4 ambaye hutaka wetu wote waokolewe,na kujua yaliyo kweli. ISA YA 60:12 KWA MAANA KILA TAIFA NA UFALME WA WATU WASIOTAKA KUKUTUMIKIA WATAANGAMIA;NAAM,WATAHARIBIWAKABISA.Bwana asifiwe! wapendwa watu wa Mungu tuombee Taifa letu zuri la Tanzania,MITHAL 11:14 PASIPO MASHAURI TAIFA HUANGUKA;BARI KWA WINGI WA WASHAURI HUJA WOKOVU.tumwombee Rais wa inchi Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan; tumwombee Mkamu wa Rais Mheshimiwa Filippo mpango, tumwombee Waziri Mkuu Mheshimiwa Majaliwa Majaliwa;tuwaombee mawaziri wote
 Tuwaombee Wabunge wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.wakuu wa mikoa wakuu wa wilaya wote viongozi wote waserikali inchini.tuwaombee watanzania wote, Tuwaombee maaskofu Wakuu,maaskofu wa majimbo,au mikoa maaskofu,wa wilaya na Wachungaji wote.Tuliombee kanisa la Mungu Tanzania.MITHALI 12:10-11, WENYE HAKI WASTAWIPO,MJI HUFURAHI;WAOVU WAANGAMIAPO,WATU HUPIGA KELELE.11 MJI HUTUKUZWA KWA MBARAKA WA MWENYE HAKI.YOHELI 2:17 HAO MAKUHANI,WAHUDUMU WA BWANA,NA WLIE KATI YA PATAKATIFU ​​NA MADHABAHU,NAACH,WASEME,WASEME, WALA USIUTOE URITHI WAKO UPATE AIBU,HATA MATAIFA WAWATAWALE JUU YAO;KWANI WASEME,KATI YA WATU,YUKO WAPI MUNGU WAO? 18 HAPO NDIPO BWANA ALIPOONA WIVU KWAAJILI YA INCHI YAKE AKAWAHURUMIA WATU WAKE.19 BWANA AKAJIBU,AKAWAMBIA WATU WAKE;TAZAMENI,NITAWALETEA NAFAKA,NA DIVAI,NA MAFUTA,NANYI MTASHIBA KWA VITU HIVYO;WALA SITAWAFANYA WAKE; LA KASKAZINI NITALIONDOLEA MBALI NANYI,NAMI NITALIFUKUZA MPAKA INCHI YA UKAME NA UKIWA;SEHEMU YAKE YA MBELE ITAINGIA KATIKA BAALI YA MAGHARIBI;NA UVUNDO WAKE UTAPANDA JUU,NA HARUFU YAKE MBAYA ITAPANDA JUU,KWA SABABU AMETENDA MAMBO. 21 Ee INCHI USIOGOPE; FURAHI NA KUSHANGILIA, KWA KUWA BWANA AMETENDA MAMBO MAKUBWA.AMEN! ungependa kuwasiliana nami kwa ushauri na maombi karibu Nipigie kwa 0612083598 au niandikie pastorvictorykiluguma@blogspot.com Amen Bwana awabariki sana


 

Monday, July 22, 2024

MKUTANO WA INJILI IRINGA


 
AGAPE PENTECOSTE JERUSALEMU CHRISTIAN CENTRE KITAYAWA IRINGA.KWA ASKOFU VICTORY KILUGUMA. TUNAYOFURAHA KUWAKALIBISHA NYOTE KATIKA MKUTANO MKUBWA WA INJILI  UTAKAOFANYIKA TAR 8/8/2023/HADI TAR 11/8/2023  BWANA AWABARIKI SANA


Tuesday, July 16, 2024

WOKOVU SEHEMU YA PILI


 Bwana Yesu akubariki ni mimi mtumishi wa Mungu victor kiluguma karibu tuendelee na sehemu ya pili ya somo letu ujue wokovu;  Wokuvu tunaupata kwa Neema ya Mungu.wokovu hatupati kwa kujitahidi kwetu kufanya matendo mema,mbele za Mungu na wanadamu, Tito 3:4-7 Mungu anatuona sisi kuwa sisi tu Roho moja na Bwana Yesu 1kor 6:17 lakini yeye aliyeungwa na Bwana ni Roho. . moja naye. sababu hii sisi tu watoto wake tumepatikana kwa kifo cha Yesu msalabani. ile damu ya thamani ya mwana wa Mungu Yesu imetutakasa na kutufanya wa thamani mbele za Mungu 1pet 1:18-19. Zaburi 2:8. Tulipo okoka tumepewa mamlaka ya kutumia jina la Yesu. Wafilipi 2:9-11. sisi tu mali ya Mungu na vyote tulivyo navyo. 1kor 6:19-20,1kor 4:1-2 baada ya kuokoka tu mawakili wa siri za Mungu. Maombi: kwa nini tuombe? Mungu anatupenda hata akatuokoa kwa neema yake kuu hawezi kutupa mahitaji yetu sisi kuomba? Mungu anajua mahitaji yetu yote hata hatujanwsmbia Mungu anatupenda sana. Kwa nini basi asitupe tu mahitaji yetu? Mbona anataka sisi tumwombe? Yafuatayo ni majibu ya maswali haya ambayo naamini wengi wanajiuliza. Bwana YESU ametufundisha tuombe Bwana atafanya Luk 11:9-10 Bwana Yesu mwenyewe alimwomba Mungu sana apewe nguvu na Mungu baba ili akamilishe huduma ya ukombozi wa mwanadamu hapa duniani. Waebr 5:7-10 tunasoma Yeye siku hizo za mwili wake alimtolea yule, aweza kumwokoa na kumtoa katika mauti,maombi na dua pamoja na kulia sana kwa machozi,akisikilizwa jinsi alivyokuwa mcha Mungu;na ingawa ni mwana,alijifunza kutii kwa mateso hayo yaliyompata; naye alipokwisha kukamilishwa,akawa sababu ya wokovu wa milele kwa watu wote wanaomtii;kisha ametajwa na Mungu kuwa Kuhani Mkuu kwa mfano wa melkizedeki. Matendo 6:4 na sisi tutadumu katika kuomba na kulihudumia lile neno. Tudumu katika kuomba kama Bwana YESU na mitume walivyo omba. Yakobo 5:16 kuomba kwake mwenye haki kwafaa sana,akiomba kwa bidii. Jinsi ya kuomba: tunaombaje? tunaomba kwa imani kutoka ndani ya Roho, si kwa maneno ya mdomoni yaliyopangwa vizuri kiakili tu, mat 6:6 maneno yanayotoka mdomoni yanatuunganisha na Mungu anayeyasikiya pia tunaweza kuomba kwa sauti kubwa ya kusikika tukiwa pekee yetu, au tukiwa wengine kama kanisani tukiomba pamoja. , Matendo 4:24 . Mungu si mwanadamu hata akachanganyikiwa kwa maombi ya watu wengi pamoja wakati mwingine wakimwomba Mungu kila jambo tofauti alivyo wa ajabu kila mmoja humsikia ombi lake na kumjibu kwa majira yake, hata kama wengine wanaomba huko ulsys,Asia,America na Africa. mbalimbali kwa wakati mmoja Mungu huwasikia wote kwa wakati mmoja. Je naweza kuomba kwa sauti ndogo sana ambayo wengine hawasikii isipokuwa mimi tu,na Mungu akanisikia? Jibu ni ndiyo. 1Samwer 1:10-17 yapo mazingira yanayotulazimu tuombe kwa sauti ndogo.Mungu hatusikii kwa kuwa tumeomba kwa sauti ndogo au kubwa. Mungu anatusikis kwa sababu tumeomba kwa imani. Je nasikia kuomba kwa kulia machozi hivi ni sawa jibu ni sawa kabisa. Bwana wetu Yesu aliomba kwa machozi kwa kulia sana. Ebra 5:7-9. Tusiogope kuwa wetu watasema nini tuombe tu kwa imani tufaham kuwa Mungu hutusikis na kutujibu. Shalom naamini somo hili limefanyika baraka kwako mtu wa Mungu naamini unachukua hutua kuwa mwombaji wa kiwango cha juu cha imani ndani ya Yesu kristo. nami nakuombea Bwana akusikie na kujibu maombi yako in Jesus name. ni mimi ushindi kiluguma bishop from lringa Tanzania karibu kwa somo lijalo na Mungu akubariki sana shalom kwa maombi na ushauri tuwasiliane kwa simu 0612083598 au pastorvictorykiluguma@blogspot.com                                                                

Monday, July 15, 2024

UJUE WOKOVU


UJUE WOKOVU:                       
shalom ni mimi mchungaji victor ninayo furaha kubwa kukuletea ujumbe wa baraka yaani ujue wokovu.                                         Tunapojifunza kukulia wokovu ni muhimu sana kuelewa maana ya wokovu wenyewe. Wokovu ni tendo la Mungu kwetu sisi wanadamu na sio sisi wanadamu kujiokoa wenyewe.mpendwa mtu wa Mungu WARUMI 10:9-10                     imeandikwa kwa sababu ukimkiri Yesu kwa kinywa chako cha kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako kuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka. . 10 kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu.            Kwa hiyo kama Mungu mwenyewe asipotuokoa sisi kwa Neema yake, kamwe hatuwezi kuokoka. HATUA YA KUAMINI NA KUKIRI                    ili uweze kukiri na  kuamini   na kukiri, imetupasa kusikia Neno la Mungu. Mpendwa mtu wa Mungu WARUMI 10:17, imeandikwa Basi imani chanzo chake ni kusikia: na kusikia huja kwa Neno la kristo. Tunaposikia Neno la kristo ndani yetu kunaumbika imani ya kristo. WARUMI 8:1,10:8-10, 2KOR 7:10.                                            HATUA YA KUPOKEA MSAMAHA WA DHAMBI                                                . Baada ya kutubu mbele za Mungu imetupasa kuamini kuwa Mungu ametusamehe dhambi zetu zote kabisa.Hakumbuki tena, nasisi tusiendelee kuzikumbuka EZEKIEL 18:21-22, imeandikwa,  lakini mtu mbaya akighairi, na kuacha dhambi zake zote alizozitenda, na kuzishika amri zangu zote, na kutenda yaliyo halali na haki, hakika ataishi, hatakufa, dhambi zake zote alizozitenda hazitakumbukwa juu yake hata mmoja; katika haki yake aliyoitenda ataishi. Haleluya! Bwana Yesu asifiwe. Tujue sasa kuwa hatuna hukumu kwa ajili ya dhambi tena 1YOH 1:9-10  tunapo jua tumemkosea Mungu kwa kufanya dhambi,hapo inakupasa kutubu kwa Mungu upesi,na Mungu mwenye Rehema atakusamehe 1YOH 1:9.                  TAHADHARI:                                             WAEBRANIA 6:4-6. Imeandikwa  kwa maana hao waliokwisha kupewa nuru,na kuonja kipawa cha mbinguni, na ushirika wa Roho matakatifu,na kulionja Neno zuri la Mungu,na nguvu za zamani za baadaye,wakaanguka baada ya hayo,haiwezekani kufanya upya tena hata watubu; kwa kuwa wamsulubisha Mwana wa Mungu mara ya pili kwa nafsi zao,na kumfedhehi kwa dhairi. KUFANYIKA KUWA MTOTO WA MUNGU. Tufahamu kuwa tunafanyika watoto wa Mungu kwa nguvu za Mungu mwenyewe, yaani Mungu mwenyewe anatufanya watoto wake. Hatuwezi kujifanya watoto wa Mungu. Mpendwa mtu wa Mungu YOHANA 1:12 imeandikwa Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake. Mpendwa mtu wa Mungu naamini somo hili limefanyika baraka kwako. Basi tukatane wakati mwingine nitakapo letea sehemu ya pili ya somo hili Bwana akubariki sana! Ni mimi victor kiluguma askofu kutoka agape pentecoste lringa Tanzania. Kwa maombi na ushauri tuwasiliane kwa blog hii pastorvictorykiluguma@blogspot.com   au kwa gmail:victorykiluguma80@gmail.com au kwa simu 0612083598.             

Monday, July 8, 2024


MPANGO WA MUNGU KUKUFANIKISHA NA KUKUSTAWISHA. ZEKARIA 1:17. piga kelele tena na kusema, Bwana wa majeshi asema hivi, kwa kufanikiwa itaeneza huko na huko tena; Naye Bwana ataufajili sayuni tena,atauchagua yerusalemu tena. ZABURI 122:6-9 utakieni yerusalemu amani na wafanikiwe wakupendao amani na ikae ndani ya kuta zako na kufanikiwa ndani ya majumba yako. Kwa ajili ya ndugu zangu na Rafiki zangu. Niseme sasa amani ikae nawe kwa ajili ya nyumba ya Bwana Mungu wetu. ZABURI 35:27 washangilie na kufurahi, wapendezwao na haki yangu. Naam waseme daima atukuzwe Bwana, apendezwae na amani ya Mtumishi wake. AYUBU 36:11. Kama wakisikia na Kumtumikia watapisha siku zao katika kufanikiwa, na miaka yao katika furaha. YOSHUA 1:8 kitabu hiki cha torati kisiondoke kinywani mwako,bali tafakari maneno yake mchana na usiku, upate kuangalia na kutenda sawasawa na maneno yote yaliyoandikwa humo; maana ndipo utakapoifanikisha njia yako,kisha ndipo utakapo sitawi sana. HALELUYA NAAMINI UJUMBE HUU UMEFANYIKA BARAKA KWAKO MSOMAJI MTU WA MUNGU BWANA AKUBARIKI NAMI NAKUOMBEA UFANIKIWE NA KUSITAWI KWA JINA LA YESU KRISTO. MUNGU ALIE HAI MUUMBA NA MWOKOZI AKATHIBITISHE NENO LAKE KATIKA MAISHA YAKO. BWANA AKUBARIKI SANA IWAPO UNEPENDA USHAURI AU MAOMBI TAFADHALI NIANDIKIE KWA GMAIL: winningkiluguma80@gmail.com au nipigie kwa 0612083598 au kwa blog hii pastorvictorykilugumablogspot