Pastor victory kiluguma blog
Wednesday, October 30, 2024
Tuesday, October 8, 2024
MWAKA WA 587 K.K.

Shalom wapendwa watu wa Mungu ni mimi pastor victory karibu tujifunze pamoja Neno la Mungu Amen! Mwaka 587 k.k Babeli walibomoa mji wa Jerusalem,wakauharibu ufalme wa Yuda wakateka nyara mali yote na kuwapeleka watu waliofaa kifungoni huko Babeli, 2fal 25:1-21. Baada ya ufalme wa Yuda kuharibiwa wakamweka Gedalia,mwana wa afisa mmoja huko Yerusalemu awe mtawala wa wenyeji wa Yuda waliobaki nchini 2fal 25:22 taz.Yer 26:24. Ufalme mpya uliweka makao yake makuu mispa kaskazini mwa Yerusalemu.na kwa msaada wa nabii Yeremia,alifuata siasa ya kujikabidhi na kutii amri ya watu wa Babeli.hivyo hakuchukua hatua dhidi ya viongozi wa kijeshi wa Yuda waliotoroka kifungoni na waliowapinga wa Babeli,bali aliwatia moyo pamoja na watu wengine wa Yuda waliotoroka kutoka kifungoni ili wahamie karibu na mispa 2fal 25:23-24 tz.Yer 40:5-12. Jemedari mmoja wa jeshi la zamani la Yuda,jina lake Ishmaeli,huyu alipinga siasa ya kuwatii babeli akafanya njama ya kumpindua Gedalia. Gedalia alipoambiwa habari zile hakuamini. Ishmael akamwinukia Gedalia pamoja maafisa wengine wa kiyahudi na wababeli waliokuwa makao makuu ya inchi.tz 2fal 25:25;Yer 40:13-41:3 huo ukawa mawazo wa mfululizo wa matukio yaliyoleta hofu kwa wayahudi wakaogopa sana kisasi cha wababeli ndipo wayahudi waliobaki wakakimbilia Misri tz 2fal 25:26;Yer 41;4-43:13. Katika biblia tunaona watu wengine wanne walioitwa Gedalia. Mfano; wa kwanza alikuwa mtaalamu wa muziki wakati wa Daudi tz 1nyak 25:3,9. Wa pili alikuwa babu wa nabii Sefania tz Sef 1:1,wa tatu alikuwa afisa wa Yerusalemu aliyempinga Yeremia,tz Yer 38:1-6 na wa nne alikuwa Kuhani wakati wa Ezra tz Ezra 10:18. Bwana akubariki kwa kufuatana nami katika somo hili Bwana awabariki sana. Ungependa kuwasiliana nami kwa ushauri maombi na maombezi karibu tuwasiliane kwa: pastorvictorykilugumablogspot.com au 0612083598.pia napenda kuwakaribisha kwa ujenzi wa kanisa hapa lringa Agape pentecoste church unaoendelea kwa bishop victory kiluguma tunapokea sadaka ya mchango wako kwa akaunt namba NMB BANK 60510090270 au Halopesa 0612083598 victory kiluguma. Nyote mnakaribishwa.
Friday, September 13, 2024
MAFUNZO YA UONGOZI NI MSINGI MKUBWA KATIKA KUJENGA MAISHA BORA YA KIKRISTO
Shalom wa pendwa katika Yesu kristo mwokozi wetu. Kitabu cha kwanza na cha pili cha Timotheo ni vitabu vinavyo funua ukweli kuhusu uongozi wa kichungaji. Nyaraka hizi mbili zinatuonesha wachungaji watumishi wa Yesu kristo ambao wamefundishwa na Mungu kukaa katika kweli ya Neno la Mungu. 1tim 3:15 mtume Paulo anamwambia Timotheo nakuandikia upate kujua jinsi iwapasavyo watu kuenenda katika nyumba ya Mungu, iliyo kanisa la Mungu aliye hai, nguzo na msingi wa kweli. Mtume Paulo anasema na mambo yale uliyoyasikia kwangu mbele ya mashahidi wengi, hayo uwakabidhi watu waaminifu watakaofaa kuwafundisha wengine " 2tim 2:2. Katika safari ya kwanza ya umisheni,Paulo alienda katika mji uitwao listra. Huko alikuwako kijana aliyekuwa akiishi huko aliitwa Timotheo. Paulo mtume akakutana naye kijana Timotheo pamoja na familia yake. Bibi na mama yake Timotheo familia hii walimpokea kristo kuwa mwokozi wao.baadae tena katika safari ya tatu huko listra mtume aliitembelea familia ya Timotheo na kumwalika Timotheo kuungana naye katika safari zake za umisheni. Timotheo akiwa kijana mkubwa alikubali kuwa mmishenari pamoja na Paulo mtume, Paulo akamwita Timotheo nakuwa kijana wake Paulo katika imani maana, alimwongoza kumfahamu Bwana. Paulo mtume alimpenda kijana Timotheo alikuwa kijana aliye mwamini Mungu imani iliyotokana na bibi yake na mama yake 2tim 1:5- baadae anajifunza kumtumikia Bwana kutoka kwa Baba wa kiroho mtume Paulo. Timotheo alikuwa na mwonekano mzuri kwa watu waliomwani Mungu katika mji wa listra na watu walimshuhudia mema. Mate 16:2 baadae sana mtume paulo akiwa gerezani anamwandikia waraka akikumbuka huruma na upendo wa kweli aliokuwa nao kijana Timotheo. mtume Paulo alifurahi mno alipomkumbuka Timotheo. 2tim 1:4. Baadae Paulo anatoka gerezani anamchukua Timotheo anamfundisha kumtumikia Bwana anasafiri naye katika huduma. Timotheo anamwona mtume Paulo akihubiri injili na kufundisha wakristo wapya. na kuwaongoza katika kweli yote ya Mungu. Timotheo anamwona mtume Paulo ni baba wa kiroho na Mwalimu wake wa imani. Mtume Paulo alifungua makanisa mapya, akiwafundisha wakristo wachanga kiroho akiwaimarisha katika imani na kuwaongoza. Mtume Paulo anamwona Timotheo ni kijana anaye penda kujifunza,anafuata kanuni ya imani, ni mwaminifu,katika mafundisho, mtume Paulo anamweka Timotheo kuwa mchungaji wa kanisa la efeso. Kazi ya Bwana aliyo kabidhiwa Timotheo ilikuwa ikiendelea kukua, Paulo na Timotheo wakaendelea kumtumikia Mungu pamoja kwa upendo kama baba na mwanae. Katika imani ya kristo. Timotheo alibaki katika mji wa efeso akifundisha na kuchunga kundi la Mungu. katika siku zile kulikuwa na hatari maana walitokea watu waliojifanya waalimu wa uongo 1tim 1:6-7 waliamu hawa walifundisha uongo. Kwa sababu hii alihitajika mtu ambaye angeweza kuwazuia, na kufichua hila yao, kwa kuwafundisha watu wa Mungu Neno la Mungu kwa usahihi kabisa.ili watu wote waijue kweli yote ya Mungu. Paulo anamwona mchungaji Timotheo angeweza kufanya hivyo. 1 tim 1:3-4. Mtume Paulo anasisitiza wetu waishike ile imani ya kweli. Ni jukumu la kila mchungaji kuliongoza kanisa, katika kweli, ya yote ya Mungu. Ni lazima mchungaji aihubiri injili ya kweli kwa uaminifu, na zaidi sana lazima mchungaji aiishi hiyo kweli mbele za Mungu na watu anaowaongoza. Haleluya! watu wa Mungu! Naami ujumbe huu utafanyika baraka kwako! Bwana awabariki nyote. Mtayarishaji ni mimi mtumishi wa Mungu Victory chalres kiluguma kutoka Agape sanctuary christian pentecoste Jerusalem lringa. Ungependa kuwasiliana nami niandikie; pastorvictorykiluguma@blogspot.com au victorykiluguma80@gmail.com au nipigie simu 0612083598. Amen!Sunday, September 1, 2024
Wednesday, August 28, 2024
MIKUTANO YA INJILI MWEZI WA 8
Shalom watu wa Mungu Mungu ni mwema namtukuza Bwana mno ametusaidia kuwa na mfululizo wa mikutano ya injili, Agost, lringa kitayawa mikutano miwili, lringa Kilolo mkutano mmoja, mkoa wa Kilimanjaro tumekuwa na mkutano mkubwa wa injili, wa siku 5 njia panda ya himo stand, na sanya juu nasai mkutano wa kufungua tawi la New life Himo kwa siku 3 na ufunguzi wa Kituo kikuu cha New life Tanzania prayer centre Himo kwa mchungaji Rafael. Amen Bwana awabariki nyote! Ni mimi victory kiluguma askofu wa Agape sanctuary Pentecostel lringa Centre Kitayawa. Kwa mawasiliano: pastorvictorykiluguma@blogspot.com. au nipigie 0612083598 au niandikie victorykiluguma@gmail.com.
Sunday, August 18, 2024
GOD BLESS YOU ALL
Thursday, August 15, 2024
AGAPE SANCTUARY CHURCH'S INTENATIONAL PENTECOSTEL JERUSALEMU CHRISTIAN CENTER IRINGA
Wednesday, August 7, 2024
MKUTANO WA INJILI UNAENDELEA

Tunamshukuru Mungu leo jumatano ni siku ya 3 tangu mkutano uanze hapa lringa kitayawa katika viwanja vya Kanisa la Agape sanctuary Pentecostel kwa askofu victory kiluguma.wachungaji wa makanisa ya kipentekoste wanashiriki mkutano huu wa Baraka tunamwona Mungu watu wanaokolewa wanafunguliwa na kuponywa na Bwana Yesu. Utukufu kwa Mungu wetu. Nyote mnakaribishwa shalom.ni mimi mtumishi victory kiluguma askofu. Karibuni sana!
Thursday, August 1, 2024
Tuesday, July 30, 2024
TUOMBEE TAIFA LETU TANZANIA
![]() |
Tuwaombee Wabunge wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.wakuu wa mikoa wakuu wa wilaya wote viongozi wote waserikali inchini.tuwaombee watanzania wote, Tuwaombee maaskofu Wakuu,maaskofu wa majimbo,au mikoa maaskofu,wa wilaya na Wachungaji wote.Tuliombee kanisa la Mungu Tanzania.MITHALI 12:10-11, WENYE HAKI WASTAWIPO,MJI HUFURAHI;WAOVU WAANGAMIAPO,WATU HUPIGA KELELE.11 MJI HUTUKUZWA KWA MBARAKA WA MWENYE HAKI.YOHELI 2:17 HAO MAKUHANI,WAHUDUMU WA BWANA,NA WLIE KATI YA PATAKATIFU NA MADHABAHU,NAACH,WASEME,WASEME, WALA USIUTOE URITHI WAKO UPATE AIBU,HATA MATAIFA WAWATAWALE JUU YAO;KWANI WASEME,KATI YA WATU,YUKO WAPI MUNGU WAO? 18 HAPO NDIPO BWANA ALIPOONA WIVU KWAAJILI YA INCHI YAKE AKAWAHURUMIA WATU WAKE.19 BWANA AKAJIBU,AKAWAMBIA WATU WAKE;TAZAMENI,NITAWALETEA NAFAKA,NA DIVAI,NA MAFUTA,NANYI MTASHIBA KWA VITU HIVYO;WALA SITAWAFANYA WAKE; LA KASKAZINI NITALIONDOLEA MBALI NANYI,NAMI NITALIFUKUZA MPAKA INCHI YA UKAME NA UKIWA;SEHEMU YAKE YA MBELE ITAINGIA KATIKA BAALI YA MAGHARIBI;NA UVUNDO WAKE UTAPANDA JUU,NA HARUFU YAKE MBAYA ITAPANDA JUU,KWA SABABU AMETENDA MAMBO. 21 Ee INCHI USIOGOPE; FURAHI NA KUSHANGILIA, KWA KUWA BWANA AMETENDA MAMBO MAKUBWA.AMEN! ungependa kuwasiliana nami kwa ushauri na maombi karibu Nipigie kwa 0612083598 au niandikie pastorvictorykiluguma@blogspot.com Amen Bwana awabariki sana
Monday, July 22, 2024
MKUTANO WA INJILI IRINGA
AGAPE PENTECOSTE JERUSALEMU CHRISTIAN CENTRE KITAYAWA IRINGA.KWA ASKOFU VICTORY KILUGUMA. TUNAYOFURAHA KUWAKALIBISHA NYOTE KATIKA MKUTANO MKUBWA WA INJILI UTAKAOFANYIKA TAR 8/8/2023/HADI TAR 11/8/2023 BWANA AWABARIKI SANA




















